MAGIX ENGA AMVAA ARROW BOY KISA GHARAMA ZA VIDEO YA “FASHIONISTA”

You are currently viewing MAGIX ENGA AMVAA ARROW BOY KISA GHARAMA ZA VIDEO YA “FASHIONISTA”
  • Post category:Burudani

Mtayarishaji wa muziki nchini, Magix Enga amenukuliwa akimuita msanii wa muziki nchini, Arrow Boy ‘mshamba’ baada ya msanii huyo kutaja gharama za video ya wimbo wake mpya, uitwao ‘Fashionista’.

Arrow Boy alisikika katika mahojiano na kituo cha redio cha humu nchini  akidai kuwa video ya wimbo wake huo  imegharimu shillingi millioni 2.2.

Mbali na kumuita Arrow Boy, mshamba katika video hiyo, Magix Enga pia aliweka mtandaoni screenshot ya mazungumzo aliyofanya miezi kadhaa na msanii huyo bila majibu akimtaja kuwa alishindwa kulipia gharama za huduma za studio alizompa.

Hata hivyo Arrow Boy amekana madai yaliyoibuliwa na Magix Enga akisema  kuwa hayana msingi wowote ikizingatiwa kuwa alishalipa gharama zote za kutayarisha wimbo wake wa “Fashionista” kuanzia audio hadi video.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa