LADY JAYDEE AACHIA ALBUM YAKE MPYA IITWAYO “20”.

You are currently viewing LADY JAYDEE AACHIA ALBUM YAKE MPYA IITWAYO “20”.
  • Post category:Burudani

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo Fleva, Judith Wambura maarufu kama Lady Jaydee ameachia rasmi album yake mpya iitwayo  ’20’.

Lady Jaydee ambaye ni moja kati ya wasanii waliyoupa muziki wa Tanzania thamani, ameachia album yake hiyo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 20 ya uwepo wake kwenye  kiwanda cha muziki wa Bongofleva.

Album hiyo inayopatikana kwenye platforms mbalimbali za kusambaza muziki duniani, ina jumla ya nyimbo 20 zilizobeba uandishi wenye ujumbe na burudani.

Hata hivyo, Jaydee anaachia album yake hii ya nane ikihesabika kuwa tayari ameutumikia muziki nusu ya umri wa maisha yake mpaka sasa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa