KIWANDA CHA NYAMA CHA NASUKUTA KUINUA UCHUMI WA WAKAAZI BONDE LA UFA.

Kiwanda cha nyama cha Nasukuta iliyoko eneo la Chepareria eneo bunge la Pokot Kusini kitaleta manufaa mengi kwa wakaazi wa kaskazini mwa  Bonde la ufa

Waziri wa kilimo kaunti ya Pokot Magharibi Geofrey Lipale anasema kwa muda sasa wengi wa wananchi wamekuwa wakisafiri mwendo mrefu kuuza mifugo wao na hali hiyo imerahisishwa

Aidha amesema kupitia kiwanda hicho  wananchi watanufaika na bei nzuri kuzidisha juhudi za kupatikana kwa soko nzuri kwa mifugo,kubuni nafasi za ajira kwa vijana  na kuinua uchumi wa kaunti

Hata hivyo ameongeza kuwa kupitia biashara mipakani itachochea  ushirikiano  mwema kudumisha  amani ambayo imekuwapo kwa muda sasa

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa