KENYA YATANGAZA KUTOPOKEA MAHINDI KUTOKA TANZANIA NA UGANDA.

You are currently viewing KENYA YATANGAZA KUTOPOKEA MAHINDI KUTOKA TANZANIA NA UGANDA.
  • Post category:Biashara

Mamlaka ya Kilimo na Chakula nchini imedai uchunguzi umebaini kuwa mahindi yanayoingia kutoka Tanzania na Uganda sio salama kwa matumizi ya binadamu.

Imedai kuwa, mahindi hayo yana kiwango kikubwa cha sumu hasa aflatoxins na fumonisins ambazo zinajulikana kusababisha Saratani.

Mamlaka hiyo imedai, Sumu hizo zimesababisha vifo vya Wakenya wengi kwa miaka, hali iliyosababisha wachukue hatua ya kuacha kupokea mahindi kutoka Tanzania na Uganda.

Aidha, imesema wataendelea kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na nchi wanazoshirikiana nazo kibiashara na wanasubiri kuona washikadau wakilizungumzia tatizo hilo

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa