KENYA YAONDOA ZUIO LA KUINGIZA MAHINDI KUTOKA TANZANIA NA UGANDA

You are currently viewing KENYA YAONDOA ZUIO LA KUINGIZA MAHINDI KUTOKA TANZANIA NA UGANDA

Serikali  imefuta marufuku iliyoweka juu ya kuagiza Mahindi kutoka Uganda na Tanzania huku ikiambatanisha masharti kwenye uingizaji wa Zao hilo.

Mnamo Machi 5, Serikali ya Kenya iliweka marufuku ya kuingiza Mahindi yaliyoagizwa kutoka nje kwa lengo la kuzuia sumu inayosababisha Saratani kwa binadamu.

Moja ya sharti lililowekwa ni washikadau wote wanaoshughulika na uagizaji wa Mahindi watahitajika kusajiliwa, shehena zinazoingia lazima zifuatwe na cheti cha viwango vya Aflatoxin na Wafanyabiashara wanapaswa kutoa maelezo ya maghala yao.

Cheti kinapaswa kuonesha kwamba viwango vya Aflatoxin vinazingatia kiwango cha juu kinachohitajika cha sehemu 10 kwa bilioni.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa