KAUNTI YA TURKANA IMEPOKEA MATANKI 30 YA MAJI KUTOKA KWA MAMLAKA INAYOSIMAMIA RASLIMALI ZA MAJI YA CENTRAL RIFT KUPIGA JEKI MAPAMBANO DHIDI YA CORONA

Serikali ya kaunti ya Turkana imepokea zaidi ya  matanki 20 ya maji yenye ujazo wa lita 1500 kutoka kwa Mamlaka  inayosimamia raslimali za maji ya Central Rift ili kupiga jeki mapambano dhidi ya virusi vya corona kaunti hiyo.

Akizungumza alipopokea matanki hayo, Waziri wa Maji kaunti ya Turkana Joseph Namwar amesema matanki hayo ya maji  yatasambazwa na kuweka kwenye maeneo ya umma ili kuwasaidia wananchi kwenye zoezi la kunawa mikono kila mara kuzuia kuenea kwa virusi vya Covid-19.

Aidha Namwar amesema serikali ya kaunti ya Turkana inaendelea kuchukua hatua mbalimbali katika kupambana na ugonjwa huo kaunti hiyo ikiwa ni pamoja na kusambaza maji na vitakasa mikono au sanitizers.

Hata hivyo amewashukuru wadau hao kutokaMamlaka inayosimamia raslimali za maji ya Central Rift kwa msaada wao huku akiwataka wakaazi wa kaunti ya Turkana waendelee kushirikiana na serikali ya kaunti katika hatua zinazochukuliwa kukabiliana na ugonjwa huo.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa