KAUNTI YA POKOT MAGHARIBI YATAKIWA KUWEKEZA ZAIDI KWENYE SUALA LA KUZALISHA CHAKULA.

You are currently viewing KAUNTI YA POKOT MAGHARIBI YATAKIWA KUWEKEZA ZAIDI KWENYE SUALA LA KUZALISHA CHAKULA.

Serikali ya kaunti ya Pokot Magharibi imetakiwa kuweka mikakati zaidi ili kuzidisha uzalishaji wa chakula katika wadi mbali mbali kaunti hiyo.

Akizungumza kwenye kikao kilichowaleta pamoja washikadau mbali mbali katika eneo la KBC Lutheran, mdhamini wa kikao hicho kutoka  shirika lisilo la kiserikali k. a. s {Konrad Adenua Stiftung) na ambaye ni mkurungezi mkuu wa shirika hilo nchini Kenya, Dr. Annette Cchwander, anasema kuwa  swala la  uzalishaji wa chakula linafaa litiliwe maanani.

Kadhalika msimamizi wa miradi nchini kwenye shirika hilo bwana Duncan Odele, amesema kwamba kikao hicho kitatoa mafunzo kwa washikadau ili waeneze ujumbe huwo kwenda kwa jamii

Kulingana na Duncan, watazidi kushirikiana na serikali ya kaunti ya Pokot Magharibi ili kutafta suluhu mwafaka ya kupunguza utapia mlo kwenye wadi kadhaa kaunti hiyo.

Ikumbukwe kilele cha kikao hicho kitakuwa hapo kesho ambapo Gavana John Lonyangapuo anatarajiwa kuhudhuria.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa