JOSE CHAMELEONE ADOKEZA MPANGO WA KUACHIA ALBUM MPYA.

You are currently viewing JOSE CHAMELEONE ADOKEZA MPANGO WA KUACHIA ALBUM MPYA.
  • Post category:Burudani

Msanii nguli wa muziki nchini Uganda Jose Chameleone ambaye juzi kati aliwania wadhfa wa umeya wa jiji la Kampala ameahidi kuachia album yake mpya kama njia ya kutangaza kuwa bado yupo kwenye biashara ya muziki.

Akiwa kwenye moja ya Interview mkali huyo wa ngoma ya Bolingo ya Nzambe amesema kwa sasa yupo kwenye harakati za kuifanyia kazi album yake mpya akiwa pamoja na maprodyuza mbali mbali, hivyo mashabiki wake watarajia kuipata album hiyo hivi karibuni.

Hata hivyo amewaondolea hofu mashabiki zake kwa kusema kuwa atabaki kuwa mwanamuziki milele na hata ikitokea amefuata ndoto zake za kuwa mwanasiasa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa