JOACHIM LOW KUACHA KUINOA UJERUMANI.

You are currently viewing JOACHIM LOW KUACHA KUINOA UJERUMANI.
  • Post category:Michezo

Kocha wa Timu ya Taifa ya Soka ya Wanaume ya Ujerumani, Joachiam Low ataacha kuifundisha timu hiyo baada ya Michuano ya EURO inayotarajiwa kufanyika Juni 11 – July 11, mwaka wa 2021.

Chama cha Soka cha Ujerumani (DFB) kimesema, mkataba wa Low ulitakiwa kuisha baada ya Michuano ya Kombe la Dunia 2022 ila Kocha huyo ameomba kusitisha mapema mkataba.

Low aliiwezesha Ujerumani kushinda Kombe la Dunia 2014 huko Brazil, alianza kuinoa timu hiyo mwaka 2006 baada ya kuwa kama Msaidizi wa Jürgen Klinsmann katika timu hiyo.

Kwa siku za karibuni, Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp amekuwa akipigiwa upatu kumrithi Low kuinoa timu hiyo ingawa Klopp mwenyewe amekanusha taarifa hizo na kusema mbeleni inawezekana ila si kwa sasa.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa