JIMMY GAIT AFUNGUKA SABABU ZA KUWA SINGO

You are currently viewing JIMMY GAIT AFUNGUKA SABABU ZA KUWA SINGO
  • Post category:Burudani

Mwanamuziki wa nyimbo za injili nchini Jimmy Gait amefunguka sababu za kutoingia kwenye ndoa.

Akiwa kwenye moja ya interview Jimmy Gait amesema licha ya kutamani kuwa na familia, bado ana uvumilivu kwenye mchakato wa kumtafuta mwanamke  wa ndoto yake kwani anamini ataingia kwenye ndoa muda sahihi ukifika.

Aidha ameenda mbali zaidi na kusema kwamba kuna kipindi alikuwa  kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa kipindi cha miaka mitano akiwa na matumaini yangempelekea kuingia kwenye ndoa lakini mwisho wa siku mahusiano hayo yalivunjika.

Kulingana na Jimmy Gait, tatizo kubwa ambalo amekutana nalo ni kumpata mtu sahihi wa kuingia nae kwenye ndoa ikizingatiwa kuwa baadhi ya watu huingia kwenye mahusiano kwa faida zao za kibinafsi.

Hata hivyo Hitmaker huyo wa ngoma ya “Makuu” amesema anaamini atampata mwanamke wa ndoto yake katika siku za hivi karibu licha ya kupata shinikizo kutoka kwa watu wake wa karibu.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa