GAVANA LONYANG’APUO AIHIDI KUBORESHA UCHUMI WA KAUNTI YAKE.

You are currently viewing GAVANA LONYANG’APUO AIHIDI KUBORESHA UCHUMI WA KAUNTI YAKE.

Gavana wa kaunti ya Pokot Magharibi John Krop Lonyang’apuo amekariri msimao wake wa kuinua uchumi wa kaunti hiyo kulingana na ajenda ya serikali yake.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zaidi ya vijana 100 wa chama cha ushirika cha kifedha maarufu WEPESA katika eneo la Chepareria, Profesa Lonyang”apuo ameelezea haja ya wakaazi kaunti hiyo kujiunga na vyama vya ushirika kama njia moja ya kujikwamua kutoka lindi la umaskini sawa na kuinua uchumi wa kaunti.

Aidha Lonyang’apuo ametoa wito kwa wakulima na wafanyibiashara kutumia fursa ya chama hicho cha wepesa kuchukua mikopo ya kuendeleza na kupanua biashara zao huku akisifia utendakazi wa serikali yake ya kusaidia wenyeji.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa