EEZY AFUNGUKA SABABU ZA KUTOACHIA REMIX YA TUMBIZA SOUND”

You are currently viewing EEZY AFUNGUKA SABABU ZA KUTOACHIA REMIX YA TUMBIZA SOUND”
  • Post category:Burudani

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Eezy amefunguka sababu za kuchelewa kuachia remix ya wimbo wake wa”Tumbiza Sound” licha ya kuwepo na mkataba wa maelewano na Wizara ya Afya nchini humo.

Akiwa kwenye moja ya interview Eezy amesema kucheleweshwa kwa malipo na kutotimizwa kwa mikataba mingine ambayo wizara ya afya nchini uganda iliahidi ndio imekwamisha juhudi za kuachiwa  kwa remix ya wimbo wake wa “Tumbiza Sound.”

Ikumbukwe Wimbo wa “Tumbiza Sound” ni moja kati singles zilizopendwa na wengi  kipindi cha lockdown nchini Uganda  lakini baadae Wizara ya Afya nchini humo ilikuja ikapiga marufuku wimbo huo kwa madai kwamba inawahimiza watu kwenda kinyume na kanuni za kuthibiti msambao wa corona.

Lakini baadae maafisa katika wazira ya afya nchini uganda walifanya kikao na msanii Eezy ambapo walimuagiza kuachia remix ya wimbo wa “Tumbuiza Sound” kwa ajili ya kuwahimiza watu kufuata taratibu za kuthibiti  janga la corona.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa