DIAMOND PLATINUMZ KUTUMBUIZA KWENYE TUZO ZA MTV AFRICA NCHINI UGANDA.

You are currently viewing DIAMOND PLATINUMZ KUTUMBUIZA KWENYE TUZO ZA MTV AFRICA NCHINI UGANDA.
  • Post category:Burudani

Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ametangazwa na waandaji wa tuzo za muziki za MTV Mama 2021 kama mmoja wa wasanii watakaotumbuiza kwenye tamasha hilo.

Orodha ya wasanii watakaotumbuiza katika tuzo hizo za kimataifa ambazo kwa msimu huu zitafanyika Februari 20 nchini Uganda kwa njia ya kidigitali ilitolewa Januari 27 ikiwa na wasanii nane kutoka nchi nane tofauti ya Afrika.

Aidha majina ya wasanii nane yaliyojitokeza kwenye orodha ya watumbuizaji hao ni Diamond (Tanzania), Nasty C (Afrika Kusini), Soraia Ramos (Cape Verde), Khaligraph Jones (Kenya), Sheeba (Uganda), WizKid (Nigeria), Suspect 95 (Ivory Coast) na kundi la Calema kutoka Sao Tome.

Mbali na kuchaguliwa kutumbuiza, pia Diamond anawania tuzo hizo pamoja na wasanii wengine 7 kutoka Tanzania ambao ni Harmonize, Zuchu na kundi la muziki wa Hip Hop la Rostam.

Tuzo za MTV Mama hufanyika kila mwaka kwa ajili ya kuwatunuku wasanii wa Afrika waliofanya vizuri kisanaa kwenye mwaka husika, na safari hii itakuwa ni mara ya kwanza kufanyika nchini Uganda.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa