CINDY SANYU AWATOLEA UVIVU WASANII WANAODHANI MUUNGANO WA WANAMUZIKI NCHINI UGANDA UTAWASAIDIA KIUCHUMI.

You are currently viewing CINDY SANYU AWATOLEA UVIVU WASANII WANAODHANI MUUNGANO WA WANAMUZIKI NCHINI UGANDA UTAWASAIDIA KIUCHUMI.
  • Post category:Burudani

Staa wa muziki nchini Uganda Cindy Sanyu amewatolea uvivu wasanii ambao wanadhani kwamba muungano wa wanamuziki nchini Uganda ni jukwaa ambalo litawasaidia kiuchumi.

Akiwa kwenye moja ya interview Cindy amesema muungano huo sio shirika la misaada bali ni vuguvugu  ambalo litawaleta pamoja wasanii ili wawe na sauti moja ya kutetea muziki wa Uganda.

Hata hivyo amesema wasanii wengi  nchini Uganda hawana furaha kwa sababu muungano wa wasanii nchini humo hautoi misaada kwa wasanii, hivyo wasitegemee chakula yeyote kutoka kwake iwapo atachaguliwa kuwa rais wa muungano huo.

Ikumbukwe Cind Sanyu ambaye ni naibu rais wa muungano wa wanamuziki nchini Uganda, kwa sasa ametia nia ya kugombea kiti cha urais wa muungano huo. 

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa