CINDY SANYU ATIA NIA KUGOMBEA URAIS WA MUUNGANO WANAMUZIKI NCHINI UGANDA (UMA).

You are currently viewing CINDY SANYU ATIA NIA KUGOMBEA URAIS WA MUUNGANO WANAMUZIKI NCHINI UGANDA (UMA).
  • Post category:Burudani

Staa wa muziki nchini Uganda Cindy Sanyu ambaye ni Naibu Rais wa Muungano wa Wanamuziki nchini humo (UMA) ametangaza tena kuwania wadhfa wa urais wa muungano huo.

Cindy ambaye alijetenga na masuala ya kuwania urais wa muungano wa wasanii nchini Uganda wiki iliyopita kwa sasa amebadilisha mawazo yake na kuweka wazi  kuwa atakuwa miongoni mwa wagombea wa kiti hicho kwenye uchaguzi ujao.

Hata hivyo  amesema alichukua uamuzi huo baada ya kuwa na mazungumzo mapana na wadau wa muziki nchini Uganda,ambao walimshawishi kugombea wadhfa wa urais wa muungano wa wasanii nchini  humo ambao uliachwa wazi na msanii  Ykee Benda ambaye alijiuzulu wiki kadhaa zilizopita.

Cindy anajiunga na wasanii GNL Zamba pamoja na Sophie Nantogo ambao wametia nia ya kuwania wadhfa wa urais wa muungano wa wasanii nchini Uganda.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa