Nyota wa muziki kutoka Nchini Nigeria Burna Boy ametajwa katika orodha ya wasanii watakaotumbuiza kwenye onyesho la utoaji wa Tuzo za Grammy mwaka 2021 litakalofanyika Machi 14 mwaka huu Los Angeles, nchini Marekani
Burna Boy ni miongoni mwa wasanii wanaowania Tuzo za Grammy mwaka wa 2021 katika Kipengele ‘Best Global Music Album’.
Sanjari na hilo mwanamuziki Jhené Aiko ndiye ameteuliwa kuwa Main Host wa Sherehe hizo.
Ikumbukwe Tuzo za Grammy za 2021 awali zilipangwa kufanyika mwezi Januari mwaka huu kabla ya kuahirishwa hadi Machi kwa sababu ya ongezeko la maambukizi ya COVID-19 huko Los Angeles nchini Marekani.