BIFU LA RAPA TEKASHI 69 NA MEEK MILL LACHUKUA MKONDO MPYA.

You are currently viewing BIFU LA RAPA TEKASHI 69  NA MEEK MILL LACHUKUA MKONDO MPYA.
  • Post category:Burudani

Bifu la Rapa Tekashi 69 na Meek Mill kutoka nchini marekani linaendelea kushika kasi, Tekashi ameibuka na madai kwamba Meek Mill ametuma barua kwa Wanasheria wake akidai kuwa anafanyiwa vitendo vya uonevu (Bullying)

Kwenye barua hiyo iliyowekwa na tekashi 69  kwenye mtandao wa instagram, inamkataza tekashi kuacha kutumia video na picha za Meek Mill kwa lengo la kujinufaisha kibiashara. 

Kwenye video ya wimbo wake mpya  uitwao “ZAZA” rapa Tekashi amemdhihaki Meek Mill kwa kutumia picha yake pamoja na video inayoonesha wakizozana, bila ridhaa yake.

Hivyo wanaomba kipande hicho kilichoanzia sekunde ya 50 kuondolewa mara moja kwenye video hiyo ambayo tayari ina  zaidi ya viewers millioni 29  kwenye mtandao wa  YouTube.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa