BAND BECCA WAACHIA RASMI ALBUM YAO MPYA IITWAYO “BECA FEVER”

You are currently viewing BAND BECCA WAACHIA RASMI ALBUM YAO MPYA IITWAYO “BECA FEVER”
  • Post category:Burudani

Bendi ya muziki nchini Band Becca hatimae imeachia rasmi album yao mpya iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki wao.

Band Becca ambayo inaundwa na wasanii Carol na Becky imewabariki mashabiki wake na  album iitwayo “Beca Fever” yenye jumla ya ngoma 11 za moto, ikiwa na kolabo 5 pekee. 

Band Becca wameshirikiana na wasanii mbali mbali wa humu nchini na nje ya nchini kama Sanaipei Tande,Mimi Mars, Femi One na Fena Gitu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram,Band Becca wamesema wameachia album hiyo kwa lengo la kuwahamasisha wanawake wote kuhusiana na changamoto wanazokutana nazo katika jamiii.

Album ya “Beca Fever” ni album ya kwanza ya wasanii wa bendi hiyo ya tangu waanze safari yao ya muziki na inapatikana ‘Exclusive’ kupitia mitandao yote ya  kukisikiliza na kuuza muziki duniani kama vile Boomplay,Spotify na Apple Music.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa