ARROW BOY ADAIWA KUIBA WIMBO WA “FASHIONISTA”

You are currently viewing ARROW BOY ADAIWA KUIBA WIMBO WA “FASHIONISTA”
  • Post category:Burudani

Mkali wa muziki nchini Arrow Boy ameingia tena katika mijadala kwenye mitandao nchini  baada ya kudaiwa kuiba  idea ya wimbo wa  ‘Dede’ wa msanii  kutoka nchini Burundi aitwaye  Davis D.

Kulingana na ripoti inayosambaa mitandaoni, inadaiwa Arrow boy ametumia mdundo na ubunifu wa video wa wimbo huo kwenye wimbo wake mpya wa “Fashionista”, hivyo kuibua maswali mengi miongoni mwa wadau wa muziki nchini ambao walienda mbali zaidi na kuhoji kuwa msanii huyo amekosa ubunifu kwenye muziki wake. 

Hata hivyo Arrow Boy hajetoa tamko lolote kuhusiana na madai hayo yaliyoibuliwa na watu kwenye mitandao ikiwa ni siku chache zimepita tangu msanii huyo aingie kwenye ugomvi na magix enga mara baada ya prodyuza huyo kudai kwamba Arrow boy hakumlipa pesa mmoja wa maprodyuza wake aliyetayarisha wimbo wa fashionista. 

Ni madai ambayo Arrow Boy alizipuzilia mbali na kudai kwamba Magix Enga alitaka kutumia jina lake kujipatia umaarufu.

Robert Elim

Robert Elim better known as Mtoto wa Nyumbani Roba is a new shade of light on the mainstream radio scene! He host an Entertainment show called Interact that usually runs every Monday to Friday from 1:00 PM to 4:00 PM and Interact Extra that runs every Saturday from 10:00 AM to 1:00 PM. Follow him on Twitter and Instagram @robertchiwawa